Tuesday, August 31, 2010

Papaa On Tuesday Kama Haipo Haipo Tu!Ila Sio Rahisi Kuipotezea


Marafiki Huru hope tuko pouwa, Mara nyingi tumezoea ule msemo wa “Kama Ipo Ipo Tu” yaani kwa maana ya kwamba kama kitu ni cha kwako ni cha kwako hata ikiwaje, lakini tumesahau kabisa kuwa kuna wakati mwingine haipo na haipo kweli lakini tunahitaji hicho kitu ama mtu kwenye maisha yetu ya kila siku. Ukweli unabaki kuwa ipo lakini hatuwezi kuipata na tunahitaji iwe yetu huwezi ipotezea wakati mwingine tunajifarii kama ipo ipo lakini ukweli hiyo tunayoikosa inatuuma na sio rahisi kuipotezea kana kwamba ulikuwa huitaki.

Kuna watu tumetamani sana wawe wenzi wetu kwenye maisha na wengine walifanyika marafiki wazuri sana lakini ghafla mambo yakageuka yakawa ndivyo sivyo je unapotezea?kwa kusema kama ipo ipo?kuna wakati haipo na tunaihitaji kwa wakati huo. Tukiwa chuo nilimpendaga sana yule dada aliyekuwa nyuma mwaka mmoja, Protace aliyekuwa rafiki yangu anakumbuka sana mahusiano yangu na yule dada, wazee wa fellowship akina Rapha, Tangi J, david, Msegu, Mbarikiwa na Sebene group lote walikuwa wameanza mchukulia mama mtumishi, hahahaha Addo pamoja na Tumaini ndo waliokuja kuniambia Papaa umeingia ndiko siko kwa issue moja mbili tatu, baada ya ufuatiliaji wa issue moja mbili tatu nikabaini nimeingia choo cha kike ukweli unaachilia huku bado unahitaji unapetezea wakati bado inakuuma? Then unajifariji kama ipo ipo tu lakini kuna wakati haipo na tunaihitaji kwenye maisha. Ukikaa mbele za watu kana kwamba umeachia na unapotezea ukikaa mwenyewe just alone unagundua kama haipo kweli haipo lakini kupotezea sio rahisi.

Kuna wakati tunatamani tuhame katika ofisi tunazofanyia kazi kutokana na manyanyaso mbali mbali mengine toka kwa waajiri wetu na wengine wafanyakazi wenzetu, umewahi takwa na bosi wako??kama hujawahi usiombe zahama hiyo ikukute, kuna wakati unaumiaaaaaa, kuna wakati unaliaaaaaaa, lakini huwezi ondoka ukasema kama ipo ipo tu why?unajua kamabisa ikiwa haipo huwezi ipotezea bwana pamoja na shida lakini ndo ndo ndo si chururu. Kuna wakati tunatamani wengine kutoka kwenye relationship tulizoingia lakini kweli utoke kwa jeuri ya Kama ipo ipo?thubutuuuuuu, ikiwa haipo huwezi potezeakuwa sawa na ikiwepo. Inawezekana haijawahi kukuta tatizo kubwa kwenye maisha yako ndo maana unaongea kama utakavyo, umewahi waza siku unapofanyia kazi ukiambiwa kuwa kuanzia leo hauna kazi tena utaondoka na kuwaambia watu kama ipo ipo?lakini ukikaa mwenyewe chumbani huwezi ipotezea kuwa eti ipo unagundua kuwa ikiwa haipo huwezi jifanya ipo bado unaihitajikwa kiasi kikubwa tu kwenye maisha. Umewahi waza mchumba wako ama mpenzio siku akifa ama amkiachana kwa namna yoyote ile utajipa moyo kuwa kama ipo ipo?unaweza ukawa unajipa moyo kwenye macho ya watu but still huwezi kuvumilia moyo unaumaaaaaaaaa, kwa sisi tulio wahi experience kukataliwa katika ku-approach tunafahamu namna ambavyo sio rahisi kupotezea moyoni kuna mchakato mahususi “to let it go”. Sio rahisi kupokea taarifa ya mkeo ana ujauzito wa rafiki yako, rafiki yako unayefanya nae biashara amekula capital ya biashara baada ya kumwamini na kumpa then ukasema kama ipo ipo ...kuna wakati tunaikosa wakati tunaihitaji iwepo.
Jiulize mambo mangapi mpaka sasa yamekuwa yakikutesa wewe mwenyewe kwa kujifanya unapotezea eti kama ipo ipo lakini ukikaa mwenyewe na ukikumbuka kichwa kinazunguka na kukuuma mpaka unatamani kulia ama wengine hata kufa, ukikumbuka fedha ulizopoteza, ukikumbuka muda uliopoteza, ukikumbuka ulivyojiotolea kwa kiasi kikubwa...watu wakikuona unasema kama ipo ipo tu...but kumbuka umeshindwa ipotezea kwa sababu ukweli wa moyo kama haipo huwezi ipotezea kimya tu.

Kama ipo Ipo tu! Lakini kama Haipo Sio Rahisi Kuipotezea.

Think Differently and Make a Difference.


…//Papaa

No comments: